Quality Education for Quality Life

Thursday, February 2, 2017

MAADHIMISHO YA WIKI YA SHERIA - LUSHOTO SEKONDARI


Katika kuadhimisha wiki ya sheria nchini tanzania, wilaya ya lushoto na uongozi mzima ngazi ya mahakama ya lushoto; walipata wasaa wa kutembelea jumuiya ya sekondari ya lushoto.

Dhumuni kubwa linaloambatana na ziara hiyo ni kutoa elimu na msaada wa kisheria kwa jamii hasa wanafunzi (kundi la vijana na watoto) ambalo kwa kiasi kikubwa ni walengwa na waathirika dhidi ya makosa ya jinai, mambo ya mirathi, unyanyasaji wa kijinsia, ajira na mimba za utotoni. Aidha, ziara hii imelenga pia kutoa mafunzo na ukaribisho wa wenye uhitaji wa msaada wa kisheria kabla na wakati wapatapo matatizo ya kisheria.
Hakimu wa Mahakama ya Lushoto -Mhe. N. R. Mwaseba (Mama Mwaseba), akitoa utangulizi wa mafunzo na utoaji elimu juu ya masuala ya kisheria, walipowatembelea wanafunzi wa Lushoto Sekondari.

Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Lushoto - Mhe. Catherine madili akitoa elimu juu ya haki na wajibu wa mtoto.
Wiki hii ya sheria (kwa mwaka huu wa sheria) inaadhimishwa kwa kauli mbiu inayolenga mhimili wa mahakama na vyombo vyake kuweza kuhudumia jamii kisheria kwa haraka na ufanisi zaidi, ili kuiwezesha jamii husika kurejea katika shughuli za ujenzi wa uchumi na taifa kwa ujumla.
Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Lushoto - Mhe. Kisasila M. Saguda  pia alipata nafasi ya  kuelimisha vijana (Wanafunzi) kuhusu sheria za mirathi, sifa za warithi, kuandika wosia  na sifa za wosia kisheria.








Wanafunzi (pichani) wakifuatilia na kusikiliza kwa makini mada mbalimbali zilizowasilishwa, katika maadhimisho ya wiki ya sheria hapa Lushoto Sekondari.

Wanafunzi wa lushoto sekondari, waliandaliwa kupata mafunzo (elimu) juu ya :-
  • Mahakama na muundo wake
  • Sheria za nchi
  • Haki na wajibu wa mtoto
  • Makosa ya jinai na uhaini
  • Sheria ya mirathi na sifa za warithi
  • Mapenzi na mimba za utotoni – sheria inasemaje?
  • Sifa za wosia


Afisa wa polisi na mwendesha mashtaka wa polisi – Mahakama ya Lushoto – Bw. Asajile G. Mwaipasi, akihamasisha usikivu na kuwaanda vijana kupokea mafunzo (mada) aliyowaandalia kuwafunza, kwa njia ya nyimbo.

Afisa wa polisi na mwendesha mashtaka wa polisi – mahakama ya lushoto – Bw. Asajile G. Mwaipasi, akiwakumbusha vijana (wanafunzi) kuhusu kutokujihusisha na mapenzi na mimba za utotoni, kisha akawasomea vifungu vya kisheria vinavyokataza na kutoa adhabu juu ya makosa ya mapenzi na mimba za utotoni.

Mwisho wa semina (mafundisho) hayo, wanafunzi na walimu walipata nafasi ya kuuliza maswali mbalimbali yanayohusiana na wigo wa kisheria ili kupata ufafanuzi, tafasili sahihi, mwongozo na muhafaka kwa masuala tatanishi kisheria.



Baadhi ya wageni meza kuu (Waheshimiwa Mahakimu) wa Mahakama ya Lushoto, wakisikiliza hoja na maswali mbalimbali yaliyoibuliwa na wanafunzi, kuhusiana na mada zilizowasilshwa na masuala mengine ya kisheria. 









Makamu Mkuu wa shule ya Sekondari Lushoto - Beatrice Shemmela (Mama Shemmela) akitoa shukrani kwa niaba ya jumuiya ya walimu wa Lushoto Sekondari, kwa ziara na mafunzo yaliyotolewa kuhusiana na masuala ya sheria na jinsi ya kupata msaada wa kisheria.


Wanafunzi na jumuiya ya walimu wa sekondari ya lushoto, walishukuru na kuonyesha furaha yao kwa ziara hii iliyowapa elimu pana katika masuala sheria.  
Baadhi ya wanafunzi wa kidato cha nne (ambao ni washiriki wa mafunzo) wakiwa katika picha ya pamoja walimu na wageni (Waheshimiwa Mahakimu - Mahakama ya Lushoto), mara baada ya kupata mafunzo/elimu.



0 comments:

Post a Comment