Quality Education for Quality Life

Saturday, August 12, 2017

FURAHA YA MKULIMA – LUSHOTO SEKONDARI



Mkulima huwa na furaha awajibikapo katika hatua zote za kilimo tangu kuandaa shamba / bustani, mbegu, kupanda, kutunza na kukuza mimea yake iwe katika ubora unaostahili; aidha furaha zaidi huwa wakati wa mavuno, kutumia ama kuuza kwa tija.




Hali hii haijifichi miongoni mwa wanafunzi – wanakikundi wa elimu ya kujitegemea (EK) na uzalishaji mali wa hapa shuleni. Kwa nyakati tofauti mbali na vipindi vyao vya darasani, pia wanafunzi hupata fursa ya kujifunza na kushiriki shughuli za ujasilia mali kwa vitendo.






Sasa ni wakati wa mazumo na mauzo, baada ya shughuli mbalimbali za upandaji, ukuzaji na utunzaji wa bustani. Mavumo yapatikanayo, uweza kugawiwa kwa wanafunzi na wanakikundi ama kuuzwa na fedha ipatikanayo kuweza kusaidia baadhi ya wanafunzi wenye uhitaji wa vifaa ya kujifunzia kama vile kununua madaftali, kalamu na nyakati nyingine fedha hizo hutumika kununua mbegu, madawa na vifaa vya bustanini kama vile mipira ya maji (kumwagilia), ndoo / madumu ya maji, nk.




Vijana hufurahia sana elimu hii shirikishi ya wakiwa darasani na wakiwa nje ya darasa kwa kazi za ujuzi zaidi.

0 comments:

Post a Comment