Ilikuwa ni siku ya furaha iliyofana sana . . . ambapo kila mmoja alikuwa na tabasamu pana lililosawajika usoni mwake. Si wanafunzi . . . si wahitimu, wazazi, walimu, wageni na wanajamii waliojumuika katika mahafali hii, kila mmoja kwa nafasi yake aliweza kuonyesha furaha yake hasa kwa vijana walioandaliwa vyema wakiwa wanahitimu masomo yao na maisha yao shuleni yakifika tamati kwa mafanyikio. Siri kubwa ni nidhamu na tabia njema ya vijana hawa (wahitimu) ambayo ni kielelezo thabiti kwa kila mwanajumuiya wa lushoto sekondari wanajivunia.
QUALITY EDUCATION FOR QUALITY LIFE
The appearance of administrative buildings, classrooms, assembly ground and a smartness gardens with beautiful flowers.
QUALITY EDUCATION FOR QUALITY LIFE
This is a place where scientific experiments are done.Science subject's teachers and students, meets here and learn by doing.It is a one among three rooms of new laboratories.
QUALITY EDUCATION FOR QUALITY LIFE
STAFF ROOM: All teachers meets here to relax,to do academic debates,to organize their daily activities related to their profession and planning on how to facilitate their youths (students).
QUALITY EDUCATION FOR QUALITY LIFE
AT CLASSROOM: students in the classroom, sitting calmly and confortably; responding to do the work as instructed and facilitated by their teeacher.
QUALITY EDUCATION FOR QUALITY LIFE
SIDE VIEW: other classrooms- buildings, assembly ground and gardens of beautiful flowers.
Sunday, December 11, 2016
MIAKA KUMI: TUNAKUMBUKA MAHAFALI YA KIDATO CHA NNE 2010 LUSHOTO SEKONDARI
Ilikuwa ni siku ya furaha iliyofana sana . . . ambapo kila mmoja alikuwa na tabasamu pana lililosawajika usoni mwake. Si wanafunzi . . . si wahitimu, wazazi, walimu, wageni na wanajamii waliojumuika katika mahafali hii, kila mmoja kwa nafasi yake aliweza kuonyesha furaha yake hasa kwa vijana walioandaliwa vyema wakiwa wanahitimu masomo yao na maisha yao shuleni yakifika tamati kwa mafanyikio. Siri kubwa ni nidhamu na tabia njema ya vijana hawa (wahitimu) ambayo ni kielelezo thabiti kwa kila mwanajumuiya wa lushoto sekondari wanajivunia.
KUMBUKUMBU YA MAHAFALI KIDATO CHA NNE (LUSHOTO SEKONDARI) 2014
Hii ni kumbukumbu ya mahafali ya kidato cha nne, shule ya sekondari lushoto; iliyofanyika tarehe 18 mwezi novemba, 2014. Kumbumbu hii inaenda sambamba na maadhimisho ya miaka kumi (10) ya shule ya sekondari lushoto (tangu kuanzishwa mwaka 2006 hadi sasa mwaka 2016).
Yafuatayo ni baadhi ya matukio katika picha na video; yaliyofana katika mahafali hii, ambayo yamebaki kuwa kumbukumbu na elimu tosha kwa wadau wa elimu na jamii kwa ujumla.
Monday, December 5, 2016
SIKIA KAZI NA WAJIBU WENU . . .
Baadhi
ya wanafunzi wa kidato cha kwanza 2016, wakiwa na mwalimu Juma
Kimbute (JK)
mapema leo hapa shuleni; dhumuni ni:
- Kuwaasa kuendeleza tabia njema na nidhamu pindi watakapokuwa nyumbani / likizo.
- Kuwapa shime kujisomea na kutafuta maarifa mapya yatakayokuwa na tija kwa kwaka wao wa masomo ujao.
- Kuwakumbusha wanafunzi wajibu wao wakiwa shuleni na wakiwa nyumbani (muda wa likizo).
- Kuwapangia kazi na zamu – wakati wa likizo ili kila mmoja ajitambue na atambue muda wake na kazi yake.
TUMEKUSIKIA ............TUTAZINGATIA . . . 👂👂👂
Saturday, October 29, 2016
KILA LA KHERI WATAHINIWA KIDATO CHA NNE 2016
Safari ya maisha ya kitaaluma ya vijana hawa.........naam inatariji kutia nanga punde wanapokwenda kuandika mitihani yao ya kuhitimu kidato cha nne Novemba mosi, 2016.
Thursday, September 1, 2016
TUKIO LA KUPATWA KWA JUA - WANAFUNZI NA WALIMU WASHUHUDIA
LEO Septemba Mosi 2016, wakati mamia ya watu wa mji wa Mbeya (Rujewa) wakishuhudia tukio la kupatwa kwa jua kwa karibu asilimia tisini na nane (98%), huku wilaya ya lushoto - tanga , hususani shule ya sekondari lushoto, wanafunzi na walimu pia walipata fursa hii adhimu ya kushuhudia tukio la kisayansi na kijiografia la kupatwa kwa jua.
Ilikuwa takribani majira ya saa tano hadi saa sita mchana, wasaa ambao kwa maeneo haya (shuleni) ndipo tukio hilo lilipata kuonekana, ingawaje lilisukwasukwa na wingi wa mawingu.
Tukio hili la kupatwa kwa jua, ni somo muhimu (kwa njia ya kushuhudia na kuona mubashara pasina shaka wala kuhadithiwa) walilopata kuona na kujifunza wanafunzi wetu, na kujiongezea maarifa Zaidi hasa katika somo la jiografia.
Ilikuwa takribani majira ya saa tano hadi saa sita mchana, wasaa ambao kwa maeneo haya (shuleni) ndipo tukio hilo lilipata kuonekana, ingawaje lilisukwasukwa na wingi wa mawingu.
Tukio hili la kupatwa kwa jua, ni somo muhimu (kwa njia ya kushuhudia na kuona mubashara pasina shaka wala kuhadithiwa) walilopata kuona na kujifunza wanafunzi wetu, na kujiongezea maarifa Zaidi hasa katika somo la jiografia.
Ikumbukwe kuwa tukio kama hilo la kupatwa kwa jua lilitokea Julai 31,1962 takribani miaka 50 iliyopita na tukio lingine lilitokea Aprili 18, 1977, na wataalamu wa anga wanabainisha kuwa tukio kama hilo litatokea tena hapa nchini Mei 21, 2031.
Sunday, August 14, 2016
HONGERA WALIMU WETU - KAZI NJEMA TWAWATAKIA
Jumuiya ya walimu, wanafunzi na wafanyakazi wote wa shule ya sekondari Lushoto, wana furaha kuwapongeza Mkuu wa shule Mr. Yona K. Ndekirwa na Madam Selestine Ifanda, kwa kuteuliwa kuwa wakuu wa shule na kupangiwa vituo vyao vipya vya kazi.
WELCOME NEW LEADERS OF SCHOOL STUDENTS' GOVERNMENT [JULY 2016 - JULY 2017]
WELCOME NEW LEADERS OF
SCHOOL STUDENTS' GOVERNMENT
[JULY 2016 – JULY 2017]
&
GOODBYE THE FORMER/
RETIRED LEADERS OF
[JULY 2015 – JULY 2016]
It's a
regular, here at Lushoto Secondary School to exchange the phase of
students’ government leadership. The appropriate time for new
elections is always conducted at July on each year, where students
use that opportunity to choose their leaders, who will lead and guide
them in performing day to day school’ activities.
Saturday, July 30, 2016
JUMUIYA YA LUSHOTO SEKONDARI YAFANYA BARAZA LA SHULE
Siku ya tarehe 29 July 2016, ni siku ya pekee sana hasa kwa jumuiya ya lushoto sekondari inayojumuisha walimu, wafanyakazi wasio walimu na wanafunzi wote; ambapo walikutana kwa pamoja ili kujadiliana na kupanga mikakati dhidi ya kumpiga adui '' UJINGA na MWENENDO MBAYA'' hasa katika mustakabali mzima wa maisha ya kitaaluma.
JUMUIYA YA LUSHOTO SEKONDARI YAFANYA BARAZA LA SHULE
Siku ya tarehe 29 July 2016, ni siku ya pekee sana hasa kwa jumuiya ya lushoto sekondari inayojumuisha walimu, wafanyakazi wasio walimu na wanafunzi wote; ambapo walikutana kwa pamoja ili kujadiliana na kupanga mikakati dhidi ya kumpiga adui '' UJINGA na MWENENDO MBAYA'' hasa katika mustakabali mzima wa maisha ya kitaaluma.
Friday, June 24, 2016
ORODHA YA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA UFUNDI KWA MWAKA 2016
KUTOKA SHULE YA
SEKONDARI LUSHOTO
ORODHA YA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA UFUNDI KWA MWAKA 2016
MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO JULAI MWAKA 2015
KUTOKA SHULE YA
SEKONDARI LUSHOTO
MAJINA YA WANAFUNZI
WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO JULAI 2015
Friday, April 22, 2016
MIAKA 10 YA SHULE YA SEKONDARI LUSHOTO - MATUKIO NA KAZI MBALIMBALI ZIFANYIKAZO
MAJARIBIO YA KISAYANSI
Wanafunzi wakiwa pamoja na mwalimu magreth msangi, wakipata maelekezo kwa jinsi ya kufanya jaribio la kisayansi katika somo la baiolojia.
Wanafunzi wakiwa tayari kufanya na
kuonyesha jaribio la kisayansi katika somo la kemia.
USAFI NA UTUNZAJI WA MAZINGIRA
Kutunza mazingira ni wajibu muhimu
katika mafunzo wayapatayo wanafunzi wawapo shuleni. Mazingira bora
yenye kutunzwa, huvutia na kuongeza hamasa kwa wanafunzi kujivuna
kuwepo mahali safi, salama na penye kuvutia.
ZIARA ZA KIMASOMO NJE YA SHULE NA NJE
YA WILAYA YA LUSHOTO
Ni utaratibu wa shule kuratibu na
kufanyikisha ziara za wanafunzi kimasomo ili kuwajengea fikra mpya na
kujifunza zaidi ya kuwapo shuleni. Hivyo kila mwaka, wanafunzi hupata
kutembelea maeneo mbalimbali kama vile mapango ya amboni -tanga,
bahari ya hindi na bandari ya tanga, mbuga na hifadhi za taifa za
wanyama pori na maeneo kadha wa kadha.
MAONYESHO YA KITAALUMA NA KAZI ZA
UBUNIFU
Mbali na kujifunza darasani, mwanafunzi
pia hupata fursa ya kuonyesha ubunifu na uwezo wa kutengeneza dhana
mbalimbali za kitaaluma, baada ya kujifunza na kufahamu jambo fulani
katika masomo yake.
Wanafunzi wakiwa katika mkusanyiko wa
asubuhi, kwa ratiba za ukaguzi wa usafi na kupokea matangazo muhimu.
UTUNZAJI WA VITALU VYA MICHE NA KUPANDA
MITI
Hapa shuleni wanafunzi wameweza
kujifunza stadi za kimazingira ikiwa ni pamoja na kuandaa vitalu ya
miche, kuikuza na kuipanda ili kutunza uoto maridhawa kuzunguka
maeneo ya eneo la shule.
MAFUNZO YA TEHAMA
Kutokana na uwepo wa vifaa vya
kompyuta, imekuwa ni fursa ya kipekee kwa wanafunzi kujiunga katika
klabu ( ICT – Skills Club) na kujifunza ujuzi mbalimbali na
matumizi ya kompyuta na programu zake.
MIKUTANO YA KITAALUMA NA BARAZA LA
SHULE
Kupitia mikutano hii na baraza,
wanafunzi wanapata fursa nzuri ya kupata ushauri, nasaha za kitaaluma
na nidhamu, kutunuku wanafunzi waliofanya vyema shuleni na pia
kutambuana kila mdau na majukumu yake shuleni.
MIDAHALO YA LUGHA YA KISWAHILI NA
KIINGEREZA
Mada hutolewa, wanafunzi nao hupata
wasaa wa kujadili na kujiandaa kwa hoja za aidha kupinga ama kukubali
hoja inayozungumziwa. Siku ya mdahalo huwa ni siku nzuri kwa
wanafunzi, kwani ni fursa yao kuonyeshana umahili wa kujenga na
kutetea hoja na hali ya kidato kimoja kushindana na kidato kingine.
Huwa inavutia sana . . .