Pages

Sunday, December 11, 2016

MIAKA KUMI: TUNAKUMBUKA MAHAFALI YA KIDATO CHA NNE 2010 LUSHOTO SEKONDARI


Ilikuwa ni siku ya furaha iliyofana sana . . . ambapo kila mmoja alikuwa na tabasamu pana lililosawajika usoni mwake. Si wanafunzi . . . si wahitimu, wazazi, walimu, wageni na wanajamii waliojumuika katika mahafali hii, kila mmoja kwa nafasi yake aliweza kuonyesha furaha yake hasa kwa vijana walioandaliwa vyema wakiwa wanahitimu masomo yao na maisha yao shuleni yakifika tamati kwa mafanyikio. Siri kubwa ni nidhamu na tabia njema ya vijana hawa (wahitimu) ambayo ni kielelezo thabiti kwa kila mwanajumuiya wa lushoto sekondari wanajivunia.

KUMBUKUMBU YA MAHAFALI KIDATO CHA NNE (LUSHOTO SEKONDARI) 2014


Hii ni kumbukumbu ya mahafali ya kidato cha nne, shule ya sekondari lushoto; iliyofanyika tarehe 18 mwezi novemba, 2014. Kumbumbu hii inaenda sambamba na maadhimisho ya miaka kumi (10) ya shule ya sekondari lushoto (tangu kuanzishwa mwaka 2006 hadi sasa mwaka 2016).

Yafuatayo ni baadhi ya matukio katika picha na video; yaliyofana katika mahafali hii, ambayo yamebaki kuwa kumbukumbu na elimu tosha kwa wadau wa elimu na jamii kwa ujumla.

Monday, December 5, 2016

SIKIA KAZI NA WAJIBU WENU . . .




Baadhi ya wanafunzi wa kidato cha kwanza 2016, wakiwa na mwalimu Juma Kimbute (JK) mapema leo hapa shuleni; dhumuni ni:


  • Kuwaasa kuendeleza tabia njema na nidhamu pindi watakapokuwa nyumbani / likizo.
  • Kuwapa shime kujisomea na kutafuta maarifa mapya yatakayokuwa na tija kwa kwaka wao wa masomo ujao.
  • Kuwakumbusha wanafunzi wajibu wao wakiwa shuleni na wakiwa nyumbani (muda wa likizo).
  • Kuwapangia kazi na zamu – wakati wa likizo ili kila mmoja ajitambue na atambue muda wake na kazi yake.







TUMEKUSIKIA ............TUTAZINGATIA . . . 👂👂👂